BREAKING: MZEE MAJUTO AFARIKI DUNIA LEO

2018-08-09 2

BREAKING: MZEE MAJUTO AFARIKI DUNIA LEO

MSANII nguli wa vichekesho Tanzania, Amri Athuman ‘Mzee King Majuto’ amefariki dunia majira ya saa 2:00 usiku huu wa Agosti 8, 2018 katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu kwa siku kadhaa.

Mtoto wa marehemu aitwaye Abuu amethibitisha kifo cha baba yake.

Pia, mchekeshaji Joti ndio wa kwanza kutoa taarifa hizo kupitia mtandao wa instagram.

“R.I.P King Majuto Umetuachia Maumivu Makubwa sana katika Tasnia ya Comedy Tanzania, sisi wanao, tutakukumbuka kwa kazi zako, upendo wako, tabasamu lako Daima milele, tulikupenda sana ila Mungu amekupenda zaidi, pumzika kwa Amani Mzee wetu,” amendika Joti.

Install GlobalPublishersApp Android: iOS: Subscribe FACEBOOK:
... TWITTER: Visit , Suazi1 WEBSITE: FACEBOOK: ... TWITTER: INSTAGRAM: ..

Free Traffic Exchange