Katika kupambana na biashara ya dawa za kulevya na upoteaji nyara za serikali Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola amemuagiza Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi nchini kuhakikisha anapatikana mbwa maalumu anayetumika katika shughuli za kupambana na uhalifu ikiwemo kunusa mabomu,dawa za kulevya,pembe za ndovu na meno ya tembo ambaye hajulikani alipo
Waziri Lugola ametoa agizo hilo leo baada ya kufanya ziara Makao Makuu ya Kikosi cha Polisi Wanamaji na Bandari na kuongeza kuwa ana taarifa kuhusu matumizi yasiyo sahihi juu ya mbwa hao ambao pia ni askari.